Upendo wa Mungu UKO KINYUME NA UBINAFSI NA ULILETWA KWETU ILI KUONDOA UBINAFSI MIOYONI MWETU!!
1 John 3:16 (New International Version)
This is how we know what love is: Jesus Christ laid down his life for us. And we ought to lay down our lives for our brothers and sisters.
16 Katika hili tumelifahamu pendo, kwa kuwa yeye aliutoa uhai wake kwa ajili yetu; imetupasa na sisi kuutoa uhai wetu kwa ajili ya hao ndugu.
1 Yohana 3:16
>> TUMEUJUA UPENDO; TULIUONA
UPENDO PALE YESU ALIPOUTOA UHAI WAKE KWA AJILI YETU
>> KWA HIVYO, NA SISI TUKIWA NA UPENDO HUO HUO MIOYONI MWETU, IMETUPASA NA SISI KUUTOA UHAI WETU KWA AJILI YA HAO NDUGU ZETU (KWA AJILI YA KANISA, AMBALO NI MWILI WA KRISTO)
>> ANAPOSEMA ' IMETUPASA' ANAMAANISHA NI LAZIMA, AMA TUNALAZIMIKA NA SISI KUUTOA UHAI WETU KWA AJILI YA NDUGU ZETU KATIKA MWILI WA KRISTO!! UKIUTOA UHAI WAKO KWA AJILI YA NDUGU ZAKO, HAKUNA KITU CHOCHOTE AMBACHO UTAWEZA KUWAZUILIA, AU KUWANYIMA, AMA KUTOWAPA!!! MAANA UMEJITOA WEWE MWENYEWE UHAI WAKO KWA AJILI YAO, UMEJITOA VYOTE VILE ULIVYO KWA AJILI YAO, NA VYOTE ULIVYONAVYO KWA AJILI YAO!! HAUNA CHAKO TENA KWA KUWA WEWE NA VYOTE ULIVYONAVYO NI MALI YAO!! KILA MMOJA KWENYE MWILI WA KRISTO AKIFANYA HIVI HAIWEZEKANI PAKAWEPO UHITAJI WA AINA YOYOTE KANISANI, KIROHO (SPIRITUALLY), KIAKILI (MENTALLY), KIHISIA (EMOTIONALLY), KIMWILI (PHYSICALLY), KIFEDHA (FINANCIALLY), KIMALI NA VITU (MATERIALLY), NA KIJAMII (SOCIALLY)
>> UHITAJI KANISANI NI ZAO LA UBINAFSI KANISANI, NA UBINAFSI KANISANI NI ZAO LA KUKOSEKANA UPENDO WA MUNGU KANISANI
1 John 5:2
[2]By this we know that we love the children of God, when we love God, and keep his commandments.
Katika hili twajua kwamba twawapenda watoto wa Mungu, tumpendapo Mungu, na kuzishika amri zake.
>> YAANI, KAMA KWELI UNAMPENDA MUNGU, NA KUZISHIKA AMRI ZAKE, LAZIMA UTAWAPENDA WATOTO WA MUNGU!! UPENDO WAKO KWA MUNGU UNAONEKANA PALE UNAPOWAPENDA WATOTO WA MUNGU!! NA HII NDIYO AMRI MPYA YA AGANO JIPYA!! HII SIYO MOJA YA ZILE AMRI KUU MBILI ZA UPENDO ZA TORATI, BALI NI AMRI MPYA!! NAYO NI:
34 Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.
Yohana 13:34
>> WATOTO WA MUNGU, WATAKATIFU, WALIO WA- KRISTO, WAMEAGIZWA KUPENDANA WAO KWA WAO, VILE VILE KAMA KRISTO ALIVYOWAPENDA!! YAANI, KILA MMOJA IMEMPASA KUUTOA UHAI WAKE KWA AJILI YA NDUGU ZAKE (1 YOHANA 3:16)
12 Amri yangu ndiyo hii, Mpendane, kama nilivyowapenda ninyi. (Yohana 15:12)
13 Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake. (Yohana 15:13)
14 Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo. (Yohana 15:14)
35 Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.(Yohana 13:35)
>> PALE KILA MKRISTO MTAKATIFU KWENYE MWILI WA KRISTO ATAKAPOUTOA UHAI WAKE KWA AJILI YA WENGINE KWENYE MWILI, NDIPO DUNIA ITAONA, NA KUTAMBUA, NA KUFAHAMU, NA KUJUA KWAMBA HUU WANAOUONA NDIO UPENDO HALISI WA KRISTO!! KAMA DUNIA INAYOLIZUNGUKA KANISA NYUMBANI, MTAANI, KAZINI, KWENYE BIASHARA, N.K. HAIWEZI KUSHUHUDIA UPENDO ULE ULE WA KRISTO KANISANI MIONGONI MWA NDUGU KATIKA KRISTO, NI DHAHIRI KANISA HILO LINAVUNJA AMRI MPYA YA YESU, NA HIYO INAMAANISHA UBINAFSI UMO KANISANI!!! JE! USHUHUDA WA JAMII INAYOKUZUNGUKA NI UPI? JE! JAMII HIYO INAONA NA KUKIRI KWAMBA HAKIKA MNAPENDANA NA NI WANAFUNZI WA YESU KWELI KWELI!!
24 Mtu asitafute faida yake mwenyewe, bali ya mwenzake.
(1 Wakorintho 10:24)
Na tena,
3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.
Wafilipi 2:3
4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.
Wafilipi 2:4
5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;
Wafilipi 2:5
DHAMBI MOYONI = UBINAFSI + CHUKI
Tukutane kwenye CHUKI!!!